Sat, 08 Jun 2024 | 10:41 PM
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji chaendelea kutoa mafunzo kwa Wahudumu wa Mabasi ya Masafa Marefu na Mijini - Dar es salaam. Mafunzo hayo ya siku sita (6) yalianza siku ya Jumatatu tarehe 03.06.2024 na kuhitimishwa siku ya Jumamosi tarehe 08.06.2024 ambapo jumla ya washiriki 43 wemehudhuria mafunzo hayo na kutunukiwa vyeti.
Akizungumza na washiriki wakati wa Hafla ya Kufunga Mafunzo hayo iliyofanyika leo katika ukumbi wa Kituo cha Ukaguzi wa Magari uliyopo katika kampasi ya Chuo Mabibo jijini Dar es salaam, Kaimu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi, Dkt. John Mahona
amewaasa washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia yale yote
waliyojifunza ili kuleta tija na mabadiliko chanya katika vituo vyao vya kazi. Amesema
"Mkayazingatie yote mliyofundishwa ili kuleta tija katika vituo vyenu vya kazi"