March 20, 2025, 9:55 a.m.
Naibu Mkuu wa Chuo - Fedha, Mipango na Utawala, Dkt. Zainabu Mshana amefungua semina ya mafunzo elekezi ya siku 3 kwa watumishi wapya ambapo amewasisitiza kufanya kazi kwa bidii, weledi, umakini, uadilifu na uaminifu ili kuhakikisha Chuo kinafikia Malengo iliyojiwekea.
Akiwa amemuwakilisha Mkuu wa Chuo (Dkt.Prosper Mgaya), Dkt. Zainabu ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kukipatia Chuo Watumishi ambao watatekeleza majukumu mbalimbali katika nyanja za Kitaaluma pamoja na Utawala. Pamoja na hayo, amewapongeza watumishi hao kwa kufaulu vizuri usaili na kupata nafasi ya kufanya kazi katika Chuo cha Taifa Cha Usafirishaji.
Aidha, amewaeleza kuwa Chuo kina matarajio makubwa kutoka kwao hivyo, semina hii ya mafunzo elekezi ni mahususi kwa ajili ya kuimarisha utendaji kazi wao ambao utazingatia maadili ya utumishi wa umma.
March 20, 2025, 9:52 a.m.
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Kasulu Kitengo cha Usalama Barabarani - Dawati la Elimu kimeanza kutoa mafunzo ya siku tano (5) ya usalama barabarani yanayolenga wanafunzi wa shule za msingi, madereva wa bodaboda, bajaji na magari madogo ya abiria wa Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.
Akizungumza na waandishi habari baada ya mafunzo hayo yaliyoanza rasmi tarehe 17.3.2025 katika shule za msingi za Murubona, Kalema, Kigamano, Umoja na Kimobwa, Mkuu wa Kituo cha
Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani - NIT, Ndg. Godlisten Msumanje amesema lengo la mafunzo hayo ni kuelimisha wanafunzi wa shule za msingi, madereva wa bodaboda, bajaji na magari madogo ya abiria kuhusu matumizi salama na sahihi ya barabara ili kusaidia kupunguza ajali na kuboresha usalama wa watumiaji wa barabara.
Kwa upande wa wanafunzi waliopatiwa mafunzo hayo wamekishukuru Chuo kwa kutoa mafunzo hayo na kuahidi kuwa mabalozi wazuri wa usalama barabarani kwa kuwaelimisha wenzao.
March 11, 2025, 11:38 a.m.
Feb. 20, 2025, 12:22 p.m.
Feb. 11, 2025, 9:31 a.m.
The National Institute of Transport (NIT) management on February 8th, 2025, visited the Prospective NIT Lindi Campus to assess the progress of the campus designated for the development of a skilled workforce and technological innovation in the Maritime, Oil, and Gas sectors. This strategic visit marks an essential step in the development of the campus toward the realization of a world-class training facility aimed at equipping professionals with the expertise needed to meet the growing demands of the maritime professionals.The campus will play a pivotal role in strengthening Tanzania's human resource capacity in this field, ensuring the workforce is equipped with cutting-edge skills to meet global standards.
The NIT delegaation included the NIT Rector, Dr. Prosper L. Mgaya, Deputy Rector for Planning, Finance and Administration Dr. Zainabu Mshana, NIT maritime experts, and NIT Estate personnel. The delegation examined the proposed Land Use Plan of the designated land for the Campus at Kikwetu, where the project is expected to take shape in the coming months.
Accompanying the NIT delegation were representatives from the consulting firm M/s Edge Engineering and Consulting Limited, who will undertake the task of designing the Phase I campus infrastructures. During the visit, the consultants were shown the proposed land where the construction of Phase I buildings and training facilities will take place, including classrooms, workshops, staff offices, and a canteen.
During the visit, NIT Rector Dr. Mgaya expressed enthusiasm about the project, emphasizing that the campus would be a game-changer for Tanzania's economy by producing highly skilled technicians and experts who can contribute to the sustainable development of the maritime industry, with emphasis on Engineering and Technology Maritime training programmes. The Campus is also expected to provide professional and short-term training programmes aimed at boosting local economies (small-scale fishing) and fostering innovation in maritime technology and resource extraction.
Furthermore, Dr. Mgaya acknowledged the profound support NIT is receiving from the Government in advancing the institution's infrastructure development agenda. He emphasized that the government's commitment to establishing the Maritime Campus in Lindi demonstrated its vision for developing local expertise in the maritime, oil, and gas sectors.
The visit concluded with a briefing from the consulting company representative on the next steps in the design phase, with a timeline set for the completion of the campus facilities.
Jan. 21, 2025, 9:54 a.m.
Jan. 16, 2025, 10:49 a.m.
Dear Esteemed NIT Stakeholders,
As we welcome the New Year, I want to take this opportunity to extend my heartfelt gratitude to each of you for your invaluable contributions to the National Institute of Transport (NIT). Your support and collaboration have played a pivotal role in our growth and success, and we are truly thankful for your commitment to our shared vision and mission.
This year is particularly special as we embark on a journey towards 2025, when we will proudly celebrate 50 years since the establishment of our Institute. This milestone is a testament to the strength of our partnerships and the impact we have made together in the Transport Sector. Together, we have made significant strides in training, research & innovation, and consultancy in the Sector.
We are excited about the upcoming 50th anniversary celebrations and the possibilities that lie ahead. Your continued engagement will be essential as we honour our past achievements and look forward to an innovative future.
On behalf of the NIT Community, I would like to wish you and your families a prosperous New Year 2025 that will bring you joy, success and health! Once again, thank you for being a vital stakeholder of the National Institute of Transport.
Jan. 16, 2025, 10:45 a.m.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya uchukuzi ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi kwa lengo la kuwatambua na kuwasajili wataalam wa Sekta hiyo.
Kauli hiyo imetolewa Desemba 20, 2024 na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe.David Kihenzile katika mahafali ya 40 ya Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), amesema bodi hiyo pia itakuwa na jukumu la kusimamia weledi na maadili ya watalaam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara.
"Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo NIT, ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Sekta ya Uchukuzi , lengo la Bodi hii litakuwa kuwatambua, kuwasajili na kusimamia weledi na maadili ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara,"amesema Kihenzile.
Amesema uanzishwaji wa bodi hiyo una lengo la kuhakikisha kazi zote za usafirishaji zinasimamiwa na watu wenye taaluma stahiki.
Akizungumzia kuhusu NIT, Kihenzile amesema Serikali itaendelea kukiwezesha Chuo ili kuhakikisha kinatimiza majukumu yake ya kuandaa wataalam, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam katika sekta ya uchukuzi kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu.
"Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, inafahamu vizuri mahitaji muhimu ya Chuo, ikiwa ni pamoja na ubora wa miundombinu ya kujifunzia, majengo, ofisi za wahadhiri na mabweni ya wanafunzi. Aidha, natambua kuwa Chuo kipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa baadhi ya miundombinu hiyo kupitia mradi wa EASTRIP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia(WB) ikiwemo mabweni ambayo nimejulishwa yamekamilika kwa asilimia 97 na majengo ya kituo cha Umahiri ya Usafiri wa Anga ambayo yamekamilika kwa asilimia 90.
"Napenda kuchukua nafasi hii kuuagiza Uongozi wa Chuo kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati ili ianze kutumika kwa kuwa mahitaji ni makubwa vilevile ninauagiza Uongozi kuendelea kutumia mapato ya ndani katika kuendeleza na kuboresha miundombinu ya Chuo,"amesisitiza Kihenzile.
Amesema amefarijika kusikia chuo kimeendelea kutanua wigo wa kutoa mafunzo katika sekta hii muhimu ya Uchukuzi, ikiwa ni pamoja na kujiimarisha katika Njia zote za Usafirishaji yaani Usafiri wa Anga, Maji, Reli, Barabara na Usafiri kwa njia ya mabomba. Mhe. Kihenzile pia amewataka wadau na wafaidika wa shughuli za chuo kwa pamoja na taasisi za umma na binafsi kuunga mkono jitihada za Chuo katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi na kuendeleza bunifu zinazozalishwa chuoni ili ziweze kutumika kwa maendeleo ya nchi.
Awali Mkuu wa Chuo cha NIT, Mhandisi Dkt. Prosper Mgaya amesema katika mahafali hayo wahitimu 4176 wametunukiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kati yao wanaume ni 2,581 na wanawake 1,595.
"Kati ya wahitimu 4176 waliohitimu 29 wametunukiwa shahada ya Uzamili, 6 wametunukiwa statashahada ya uzamili,wahitimu 3,077 wametunukiwa shahada ya kwanza,wahitimu 36 wametunukiwa stashahada ya juu huku wahitimu 909 wametunukiwa stashahada ya kawaida, wahitimu 22 astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.
Akizungumzia changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.
"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya
Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.
Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.
Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).
astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.
Akizungumzia changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.
"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya
Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.
Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.
Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).
Dec. 6, 2024, 3:57 p.m.
Dec. 3, 2024, 1:57 p.m.
50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025
Excellence in Transport for a Sustainable Economy.