National Institute of Transport - NIT

LATEST NEWS

Wed, 05 Jun 2024 | 12:08 PM

NIT NA SIMBA SUPPLY CHAIN SOLUTION YAHUISHA MKATABA WA USHIRIKIANO

National Institute of Transport - NIT

Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya (kushoto) akikabidhia vitabu na Meneja wa Kampuni ya Simba Supply Chain Solutions Ndg. Ajuaye Kheri Msese vinavyoelimisha umuhimu wa kubadili tabia kwa watumiaji wa Barabara "Mfumo Mahiri wa Msingi wa Kitabia" mara baada ya kuhuisha Mkataba wa Ushirikiano baina yaTaasisi hizo mbili, tarehe 4 Juni, 2024.

Latest News

National Institute of Transport - NIT

NIT MANAGEMENT VISITS THE PROSPECTIVE NIT LINDI CAMPUS.

Feb. 11, 2025, 9:31 a.m.

The National Institute of Transport (NIT) management on February 8th, 2025, visited the Prospective NIT Lindi Campus to assess the progress of the campus designated for the development of a skilled workforce and technological innovation in the Maritime, Oil, and Gas sectors. This strategic visit marks an essential step in the development of the campus toward the realization of a world-class training facility aimed at equipping professionals with the expertise needed to meet the growing demands of the maritime professionals.The campus will play a pivotal role in strengthening Tanzania's human resource capacity in this field, ensuring the workforce is equipped with cutting-edge skills to meet global standards.

The NIT delegaation included the NIT Rector, Dr. Prosper L. Mgaya, Deputy Rector for Planning, Finance and Administration Dr. Zainabu Mshana, NIT maritime experts, and NIT Estate personnel. The delegation examined the proposed Land Use Plan of the designated land for the Campus at Kikwetu, where the project is expected to take shape in the coming months.

Accompanying the NIT delegation were representatives from the consulting firm M/s Edge Engineering and Consulting Limited, who will undertake the task of designing the Phase I campus infrastructures. During the visit, the consultants were shown the proposed land where the construction of Phase I buildings and training facilities will take place, including classrooms, workshops, staff offices, and a canteen.

During the visit, NIT Rector Dr. Mgaya expressed enthusiasm about the project, emphasizing that the campus would be a game-changer for Tanzania's economy by producing highly skilled technicians and experts who can contribute to the sustainable development of the maritime industry, with emphasis on Engineering and Technology Maritime training programmes. The Campus is also expected to provide professional and short-term training programmes aimed at boosting local economies (small-scale fishing) and fostering innovation in maritime technology and resource extraction.

Furthermore, Dr. Mgaya acknowledged the profound support NIT is receiving from the Government in advancing the institution's infrastructure development agenda. He emphasized that the government's commitment to establishing the Maritime Campus in Lindi demonstrated its vision for developing local expertise in the maritime, oil, and gas sectors.

The visit concluded with a briefing from the consulting company representative on the next steps in the design phase, with a timeline set for the completion of the campus facilities.

 

National Institute of Transport - NIT

NIT YASHEHEREKEA MAHAFALI YA 40, BODI YA WATAALAM WA SEKTA YA UCHUKUZI KUUNDWA

Jan. 16, 2025, 10:45 a.m.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya uchukuzi ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi  kwa lengo la kuwatambua na kuwasajili wataalam wa Sekta hiyo.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 20, 2024 na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe.David Kihenzile katika mahafali ya 40 ya Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji  (NIT), amesema bodi hiyo pia itakuwa na jukumu la kusimamia weledi na maadili ya watalaam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara.

"Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo NIT, ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Sekta ya Uchukuzi , lengo la Bodi hii litakuwa kuwatambua, kuwasajili na kusimamia weledi na maadili ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara,"amesema Kihenzile.

Amesema uanzishwaji wa bodi hiyo una lengo la kuhakikisha  kazi zote za usafirishaji zinasimamiwa na watu wenye taaluma stahiki.

Akizungumzia kuhusu NIT, Kihenzile amesema  Serikali itaendelea kukiwezesha Chuo  ili kuhakikisha  kinatimiza majukumu yake ya kuandaa wataalam, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam katika sekta ya uchukuzi kwa maendeleo  endelevu ya Taifa letu.

"Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, inafahamu vizuri mahitaji muhimu ya Chuo, ikiwa ni pamoja na ubora wa miundombinu ya kujifunzia, majengo, ofisi za wahadhiri na mabweni ya wanafunzi. Aidha, natambua kuwa Chuo kipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa baadhi ya miundombinu hiyo kupitia mradi wa EASTRIP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia(WB) ikiwemo mabweni ambayo nimejulishwa yamekamilika kwa asilimia 97 na majengo ya kituo cha Umahiri ya Usafiri wa Anga ambayo yamekamilika kwa asilimia 90.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuuagiza Uongozi wa Chuo kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati ili ianze kutumika kwa kuwa mahitaji ni makubwa vilevile ninauagiza Uongozi kuendelea kutumia mapato ya ndani katika kuendeleza na kuboresha miundombinu ya Chuo,"amesisitiza Kihenzile.

Amesema amefarijika kusikia chuo kimeendelea kutanua wigo wa kutoa mafunzo katika sekta hii muhimu ya Uchukuzi, ikiwa ni pamoja na kujiimarisha katika Njia zote za Usafirishaji yaani Usafiri wa Anga, Maji, Reli, Barabara na Usafiri kwa njia ya mabomba. Mhe. Kihenzile pia amewataka wadau na wafaidika wa shughuli za chuo kwa pamoja na taasisi za umma na binafsi kuunga mkono jitihada za Chuo katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi na kuendeleza bunifu zinazozalishwa chuoni ili ziweze kutumika kwa maendeleo ya nchi.

Awali Mkuu wa Chuo cha NIT, Mhandisi  Dkt. Prosper Mgaya amesema katika mahafali hayo  wahitimu 4176  wametunukiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kati yao wanaume  ni 2,581 na wanawake 1,595.

"Kati ya wahitimu 4176 waliohitimu 29 wametunukiwa shahada ya Uzamili, 6 wametunukiwa statashahada ya uzamili,wahitimu 3,077 wametunukiwa shahada ya kwanza,wahitimu 36 wametunukiwa stashahada ya juu huku wahitimu 909 wametunukiwa stashahada ya kawaida, wahitimu 22  astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

 

National Institute of Transport - NIT

ππˆπ“ π˜π€π“πŽπ€ πŒπ€π…π”ππ™πŽ π˜π€ π”π’π€π‹π€πŒπ€ ππ€π‘π€ππ€π‘π€ππˆ πŠπ–π€ πŒπ€πƒπ„π‘π„π•π€ 𝐍𝐀 πŒπ€πŠπŽππƒπ€πŠπ“π€ πŒπŠπŽπ€ 𝐖𝐀 πŠπ”π’πˆππˆ 𝐔𝐍𝐆𝐔𝐉𝐀

Aug. 30, 2024, 9:04 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani Zanzibar (ZARTSA) kimetoa mafunzo ya usalama barabarani kwa madereva na makondakta wa gari za abiria wa Mkoa wa Kusini Unguja.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku moja (1) yaliyofanyika tarehe 21.11.2024 Dunga Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia yale yote watakayojifunza ili kuondoa changamoto ya ajali za barabarani Zanzibar ambazo zimesababisha vifo na ulemavu kwa watu wengi.

Pia Mhe. Mahmoud ameushukuru Uongozi wa Chuo kwa kutoà mafunzo ya usalama barabarani kwa madereva na makondakta wa magari ya abiria katika Mkoa wa Kusini Unguja.

Naye Mkuu wa Kituo cha
Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani - NIT, Ndg. Godlisten Msumanje amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo madereva na makondakta juu ya matumizi sahihi ya barabara.

Kwa upande wa madereva na makonda waliyopatiwa mafunzo hayo wamekishukuru Chuo kwa kutoa mafunzo hayo na kuahidi kuzingatia yale yote waliojifunza ili kuboresha utendaji wa kazi zao.

50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025

Excellence in Transport for a Sustainable Economy.