National Institute of Transport - NIT

LATEST NEWS

Fri, 30 Aug 2024 | 08:57 AM

π—‘π—œπ—§ π—¬π—”π—œπ—•π—¨π—žπ—” π— π—¦π—›π—œπ—‘π——π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—ͺ𝗔𝗑𝗭𝗔 π—žπ—ͺπ—˜π—‘π—¬π—˜ π— π—”π—’π—‘π—˜π—¦π—›π—’ 𝗬𝗔 π—žπ—’π—‘π—šπ—”π— π—”π—‘π—’ π—Ÿπ—” π—§π—œπ—¦π—” π—Ÿπ—” π—ͺπ—”π—›π—”π—‘π——π—œπ—¦π—œ π—ͺ𝗔𝗑𝗔π—ͺπ—”π—žπ—˜ π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—” (𝗧𝗔π—ͺπ—˜π—–π—˜)

National Institute of Transport - NIT

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeibuka mshindi wa kwanza (1) kati ya Taasisi kumi na moja(11) za Elimu ya Juu ambazo zimeshiriki kwenye maonesho ya kongamano la tisa 9 la wahandisi wanawake Tanzania (Tawece) na kukabidhiwa tuzo ya mshindi wa kwanza.

Kongamano hilo limefanyika jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) kuanzia tarehe 21 hadi 22 Agosti,2024.

Mkuu wa Idara ya π™€π™‘π™šπ™˜π™©π™§π™€π™£π™žπ™˜π™¨ 𝙖𝙣𝙙 π™π™šπ™‘π™šπ™˜π™€π™’π™’π™ͺπ™£π™žπ™˜π™–π™©π™žπ™€π™£ π™€π™£π™œπ™žπ™£π™šπ™šπ™§π™žπ™£π™œ Bi. Grace Kibweja amepokea tuzo hiyo ya mshindi wa kwanza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo.

Latest News

National Institute of Transport - NIT

ZIARA YA NAIBU KATIBU MKUU - UCHUKUZI

May 13, 2025, 11:44 a.m.

Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Ludovick Nduhiye  ameutaka uongozi wa chuo cha Taifa cha Usafiraji (NIT) kuhakikisha wanatunza na  kuendeleza vifaa kwa ajili ya mafunzo ya Urubani, Wahudumu wa ndani ya Ndege na Wahandisi Matengenezo ya ndege.

Nduhiye amesema  hayo tarehe 9.5.2025 baada ya kutembelea na kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Serikali katika kufundishia mafunzo ya Marubani na Wahudumu wa ndani ya Ndege.

“Serikali imewekeza fedha nyingi katika kununua vifaa hivyo vya kufundishia marubani hivyo uongozi wa Chuo unatakiwa kuhakikisha vifaa hivi vinatunzwa ili vidumu kwa muda mrefu” Alisema Nduhiye.

Pamoja na kukagua  na kutembelea vifaa hivyo pia alikagua ujenzi wa hosteli za wanafunzi wa kike na wakiume  majengo ya utawala ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 98 na unatarajiwa kukamilika katika mwaka huu.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya amesema kuwa vifaa vyote vya  kufundisha urubani katika chuo  vimekamilika na mafunzo hayo yanatarajia kuanza Mwezi sita  mwaka huu. Aidha ameushukuru Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali yote kwakuwa wamewezesha ununuzi wa vifaa hivyo.

“ Vifaa vya kufundishia Urubani vimekamilika na tumeshapata idhini kutoka mamlaka ya Usimamizi wa Anga (TCAA) kuanza kufundisha hivyo tunatarajia kuanza kutoa mafunzo haya mwezi wa sita na tuanza na wanafunzi kumi na mbili” Alisema Mgaya

 Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho Prof. Ulingeta Mbamba amesema Baraza la chuo litaendelea kusimamia  Ubora  wa Elimu unaotolewa na chuo hicho kwa masomo yaote ili chuo hicho kiendelee kutoa wataalam wanaoweza kushindana katika soko la ajira za ndani na nje ya nchi.

Mkufunzi wa Mafunzo ya wahudumu wa ndani ya Ndege amesema kuwa vifaa vyote vya wahudumu wa ndege vipo tayari kwa ajili ya kufundishia hivyo anawakaribisha  vijana   kwenda katika chuo hicho kupata mafunzo hayo katika Sekta ya Anga.

National Institute of Transport - NIT

NIT GRADUATE EXIT PROGRAMME

May 13, 2025, 11:41 a.m.

National Institute of Transport (NIT) conducted a graduate exit programme at the NIT Mabibo Campus. This programme, among other things, is designed to better prepare graduates for the employment market.
Speaking at the inauguration of the programme, the Acting Deputy Rector for Academic Research and Consultancy, Dr. Eva Luhwavi, stated that today is indeed another significant occasion in your academic careers, during which the Institute is equipping you to more effectively navigate the job market. This event elicits a range of emotions in graduating students: delight in expectation of embarking upon a new chapter in their lives and, for others, pleasure and satisfaction with their accomplishments.
"And we, as the Institute, also take pride in your achievements. Concurrently, we bear the responsibility of working tirelessly and continuing to enhance the quality of our training and to develop contemporary teaching and research methods," Dr. Luhwavi added. "I would like to take this opportunity to congratulate all the students who will graduate in this academic year of 2024/2025. You have undertaken a considerable journey here at the NIT, with some of you having spent four years and others three. I sincerely request that the time you have invested at the Institute has not been in vain, so that you may proceed to contribute effectively wherever you may go.
"We are all aware that human resources constitute one of the most crucial foundations in establishing a modern and efficient society. Therefore, I would advise all of you who are graduating to utilise the knowledge you have acquired, each within your respective discipline, to foster the development of our nation."
Dr. Luhwavi Concluded, I would implore employers and parents to give these graduates opportunities so that they may demonstrate their proficiency. There is a tendency to favour the recruitment of young individuals with prior experience. I assure you that our young people have undergone practical training, and thus, despite their potential lack of experience in a professional environment, they possess the skills necessary to apply in the roles they will secure. Indeed, I believe in their capabilities"

50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025

Excellence in Transport for a Sustainable Economy.