National Institute of Transport - NIT
Bonyeza Kuthibitisha

LATEST NEWS

Thu, 16 Jan 2025 | 10:45 AM

NIT YASHEHEREKEA MAHAFALI YA 40, BODI YA WATAALAM WA SEKTA YA UCHUKUZI KUUNDWA

National Institute of Transport - NIT

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya uchukuzi ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi  kwa lengo la kuwatambua na kuwasajili wataalam wa Sekta hiyo.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 20, 2024 na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe.David Kihenzile katika mahafali ya 40 ya Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji  (NIT), amesema bodi hiyo pia itakuwa na jukumu la kusimamia weledi na maadili ya watalaam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara.

"Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo NIT, ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Sekta ya Uchukuzi , lengo la Bodi hii litakuwa kuwatambua, kuwasajili na kusimamia weledi na maadili ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara,"amesema Kihenzile.

Amesema uanzishwaji wa bodi hiyo una lengo la kuhakikisha  kazi zote za usafirishaji zinasimamiwa na watu wenye taaluma stahiki.

Akizungumzia kuhusu NIT, Kihenzile amesema  Serikali itaendelea kukiwezesha Chuo  ili kuhakikisha  kinatimiza majukumu yake ya kuandaa wataalam, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam katika sekta ya uchukuzi kwa maendeleo  endelevu ya Taifa letu.

"Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, inafahamu vizuri mahitaji muhimu ya Chuo, ikiwa ni pamoja na ubora wa miundombinu ya kujifunzia, majengo, ofisi za wahadhiri na mabweni ya wanafunzi. Aidha, natambua kuwa Chuo kipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa baadhi ya miundombinu hiyo kupitia mradi wa EASTRIP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia(WB) ikiwemo mabweni ambayo nimejulishwa yamekamilika kwa asilimia 97 na majengo ya kituo cha Umahiri ya Usafiri wa Anga ambayo yamekamilika kwa asilimia 90.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuuagiza Uongozi wa Chuo kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati ili ianze kutumika kwa kuwa mahitaji ni makubwa vilevile ninauagiza Uongozi kuendelea kutumia mapato ya ndani katika kuendeleza na kuboresha miundombinu ya Chuo,"amesisitiza Kihenzile.

Amesema amefarijika kusikia chuo kimeendelea kutanua wigo wa kutoa mafunzo katika sekta hii muhimu ya Uchukuzi, ikiwa ni pamoja na kujiimarisha katika Njia zote za Usafirishaji yaani Usafiri wa Anga, Maji, Reli, Barabara na Usafiri kwa njia ya mabomba. Mhe. Kihenzile pia amewataka wadau na wafaidika wa shughuli za chuo kwa pamoja na taasisi za umma na binafsi kuunga mkono jitihada za Chuo katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi na kuendeleza bunifu zinazozalishwa chuoni ili ziweze kutumika kwa maendeleo ya nchi.

Awali Mkuu wa Chuo cha NIT, Mhandisi  Dkt. Prosper Mgaya amesema katika mahafali hayo  wahitimu 4176  wametunukiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kati yao wanaume  ni 2,581 na wanawake 1,595.

"Kati ya wahitimu 4176 waliohitimu 29 wametunukiwa shahada ya Uzamili, 6 wametunukiwa statashahada ya uzamili,wahitimu 3,077 wametunukiwa shahada ya kwanza,wahitimu 36 wametunukiwa stashahada ya juu huku wahitimu 909 wametunukiwa stashahada ya kawaida, wahitimu 22  astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

 

Latest News

National Institute of Transport - NIT

๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—จ ๐— ๐—ž๐—จ๐—จ ๐—จ๐—–๐—›๐—จ๐—ž๐—จ๐—ญ๐—œ ๐—”๐—™๐—จ๐—ก๐—š๐—จ๐—” ๐—ž๐—œ๐—ž๐—”๐—ข ๐—–๐—›๐—” ๐—•๐—”๐—ฅ๐—”๐—ญ๐—” ๐—Ÿ๐—” ๐—ช๐—”๐—™๐—”๐—ก๐—ฌ๐—”๐—ž๐—”๐—ญ๐—œ ๐—ก๐—œ๐—ง ๐— ๐—ž๐—ข๐—”๐—ก๐—œ ๐——๐—ข๐——๐—ข๐— ๐—”

June 27, 2025, 5:41 p.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimefanya kikao cha kawaida cha Baraza la Wafanyakazi tarehe 27 Juni, 2025 katika Ukumbi wa Midland Inn View Hotel, Dodoma. Kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika Juni 26, 2025.

Kikao hicho kilifunguliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ambaye alikipongeza chuo kwa kuandaa vikao vinavyodumisha ushirikiano wa watumishi na uongozi. Alisisitiza kuwa NIT iendelee kuzalisha wataalamu kutokana na ukuaji wa sekta ya usafirishaji unaoletwa na miradi kama SGR na ongezeko la ndege za ATCL. Aidha, alihimiza ushirikiano na vyuo vya nje kwa ajili ya maendeleo ya kiteknolojia.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, Prof. Obadia Mbamba, alishukuru Wizara kwa ushirikiano wake unaosaidia ustawi wa chuo. Viongozi wa vyama vya wafanyakazi wa THTU na RAAWU Taifa waliupongeza uongozi wa NIT kwa maandalizi bora ya kikao na kutoa motisha kwa watumishi (incentive) inayoongeza morali ya kazi.

Mkuu wa Chuo, Dkt. Prosper Mgaya, alimshukuru Prof. Kahyarara kwa kuwa mgeni rasmi na kuahidi kuendeleza vikao hivyo kwa kuzingatia sheria na kanuni husika.

National Institute of Transport - NIT

๐๐ˆ๐“ ๐˜๐€๐“๐Ž๐€ ๐Œ๐€๐…๐”๐๐™๐Ž ๐˜๐€ ๐”๐’๐€๐‹๐€๐Œ๐€ ๐๐€๐‘๐€๐๐€๐‘๐€๐๐ˆ ๐Š๐–๐€ ๐Œ๐€๐ƒ๐„๐‘๐„๐•๐€ ๐–๐€ ๐•๐˜๐Ž๐Œ๐๐Ž ๐•๐˜๐€ ๐Œ๐Ž๐“๐Ž ๐Œ๐Š๐Ž๐€ ๐–๐€ ๐๐–๐€๐๐ˆ.

June 26, 2025, 11:29 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani (RCoERS), kimeanza kutoa mafunzo maalum ya usalama barabarani kwa madereva wa magari makubwa ya mizigo, daladala na bodaboda katika Mkoa wa Pwani.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 24 Juni, 2025 katika Stendi Kuu ya Mabasi ya Kibaha, Mkuu wa Kituo cha Umahiri cha Kikanda cha Usalama Barabarani – NIT, Ndg. Godlisten Msumanje, alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo madereva hao kutekeleza majukumu yao kwa weledi, huku wakizingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kulinda usalama wao pamoja na wa abiria wanaowahudumia.

“NIT imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji nchini kutoa elimu endelevu ya usalama barabarani kwa makundi mbalimbali katika jamii ili kuongeza uelewa wa usalama barabarani kwa watumiaji wote wa barabara,” alisisitiza Ndg. Msumanje.

Mafunzo haya yalianza rasmi tarehe 23 Juni, 2025 na yanatarajiwa kukamilika tarehe 27 Juni, 2025.

National Institute of Transport - NIT

๐Ÿฎ๐Ÿฌ ๐—ง๐—”๐—ก๐—ญ๐—”๐—ก๐—œ๐—”๐—ก ๐—ฆ๐—ง๐—จ๐——๐—˜๐—ก๐—ง๐—ฆ ๐—š๐—ฅ๐—”๐——๐—จ๐—”๐—ง๐—˜ ๐—™๐—ฅ๐—ข๐—  ๐—ก๐—œ๐—งโ€“๐—ž๐—œ๐—›๐—•๐—ง ๐—๐—ข๐—œ๐—ก๐—ง ๐—˜๐—ก๐—š๐—œ๐—ก๐—˜๐—˜๐—ฅ๐—œ๐—ก๐—š

June 26, 2025, 11:25 a.m.

oday, June 24, 2025, twenty (20) Tanzanian students graduated from a six-month joint engineering program between the National Institute of Transport (NIT) and the Kenya Institute of Highways and Building Technology (KIHBT) at the NIT Mabibo Campus.

Speaking during the graduation ceremony, Dr. Prosper Mgaya, Rector of NIT, announced that NIT and KIHBT formalized their partnership by signing a Memorandum of Understanding in October 2023 in Nairobi, Kenya. This collaboration operates under the umbrella of the World Bank's East Africa Skills for Transformation and Regional Integration Project (EASTRIP). Dr. Mgaya stated that following the signing, discussions focused on implementing a student exchange and mobility program to fulfill EASTRIP's requirement for regional enrollment in long-course programs.

On his side Dr. Chacha Ryoba, Center Leader of the NIT Center of Excellence in Transport Operations under EASTRIP, elaborated on the program structure. He stated that each institution enrolled twenty students in two distinct programs: Power Train and Suspension Systems and Construction Material and Testing.

NIT students completed a one-month in-person phase of the program in Kenya, followed by five months of online instruction delivered by KIHBT lecturers. Conversely, KIHBT students completed a one-month in-person phase in Tanzania, followed by five months of online instruction delivered by NIT lecturers. While the Kenyan students graduated on June 19, 2025, the Tanzanian students received their certifications today, June 24, 2025. The graduates expressed optimism and enthusiasm for their future endeavors in the engineering field.

50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025

Excellence in Transport for a Sustainable Economy.