National Institute of Transport - NIT

LATEST NEWS

Thu, 16 Jan 2025 | 10:45 AM

NIT YASHEHEREKEA MAHAFALI YA 40, BODI YA WATAALAM WA SEKTA YA UCHUKUZI KUUNDWA

National Institute of Transport - NIT

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya uchukuzi ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi  kwa lengo la kuwatambua na kuwasajili wataalam wa Sekta hiyo.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 20, 2024 na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe.David Kihenzile katika mahafali ya 40 ya Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji  (NIT), amesema bodi hiyo pia itakuwa na jukumu la kusimamia weledi na maadili ya watalaam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara.

"Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo NIT, ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Sekta ya Uchukuzi , lengo la Bodi hii litakuwa kuwatambua, kuwasajili na kusimamia weledi na maadili ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara,"amesema Kihenzile.

Amesema uanzishwaji wa bodi hiyo una lengo la kuhakikisha  kazi zote za usafirishaji zinasimamiwa na watu wenye taaluma stahiki.

Akizungumzia kuhusu NIT, Kihenzile amesema  Serikali itaendelea kukiwezesha Chuo  ili kuhakikisha  kinatimiza majukumu yake ya kuandaa wataalam, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam katika sekta ya uchukuzi kwa maendeleo  endelevu ya Taifa letu.

"Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, inafahamu vizuri mahitaji muhimu ya Chuo, ikiwa ni pamoja na ubora wa miundombinu ya kujifunzia, majengo, ofisi za wahadhiri na mabweni ya wanafunzi. Aidha, natambua kuwa Chuo kipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa baadhi ya miundombinu hiyo kupitia mradi wa EASTRIP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia(WB) ikiwemo mabweni ambayo nimejulishwa yamekamilika kwa asilimia 97 na majengo ya kituo cha Umahiri ya Usafiri wa Anga ambayo yamekamilika kwa asilimia 90.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuuagiza Uongozi wa Chuo kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati ili ianze kutumika kwa kuwa mahitaji ni makubwa vilevile ninauagiza Uongozi kuendelea kutumia mapato ya ndani katika kuendeleza na kuboresha miundombinu ya Chuo,"amesisitiza Kihenzile.

Amesema amefarijika kusikia chuo kimeendelea kutanua wigo wa kutoa mafunzo katika sekta hii muhimu ya Uchukuzi, ikiwa ni pamoja na kujiimarisha katika Njia zote za Usafirishaji yaani Usafiri wa Anga, Maji, Reli, Barabara na Usafiri kwa njia ya mabomba. Mhe. Kihenzile pia amewataka wadau na wafaidika wa shughuli za chuo kwa pamoja na taasisi za umma na binafsi kuunga mkono jitihada za Chuo katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi na kuendeleza bunifu zinazozalishwa chuoni ili ziweze kutumika kwa maendeleo ya nchi.

Awali Mkuu wa Chuo cha NIT, Mhandisi  Dkt. Prosper Mgaya amesema katika mahafali hayo  wahitimu 4176  wametunukiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kati yao wanaume  ni 2,581 na wanawake 1,595.

"Kati ya wahitimu 4176 waliohitimu 29 wametunukiwa shahada ya Uzamili, 6 wametunukiwa statashahada ya uzamili,wahitimu 3,077 wametunukiwa shahada ya kwanza,wahitimu 36 wametunukiwa stashahada ya juu huku wahitimu 909 wametunukiwa stashahada ya kawaida, wahitimu 22  astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

 

Latest News

National Institute of Transport - NIT

ππˆπ“ 𝐋𝐀𝐔𝐍𝐂𝐇𝐄𝐒 𝐄𝐀𝐒𝐀 π“π‘π€πˆππˆππ† ππ‘πŽπ†π‘π€πŒ

Oct. 7, 2025, 5:34 p.m.

National Institute of Transport (NIT) in collaboration with Aerolink Solutions Ltd and in cooperation with the Athens Aviation Training Organization (AATO) has officially launched EASA Program at the National Institute of Transport.

The inauguration ceremony was held at NIT on 7th October, 2025 aiming at nurturing a new generation of highly skilled and internationally certified aircraft maintenance engineers.

The inauguration was officiated by Director General of Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) Mr. Salim Msangi as the guest of honor for the event. In his address during the launching ceremony Mr. Msangi congratulated the Institute for the remarkable achievement. He further stressed that NIT should continuously strive to have qualified instructors and state of art training facilities inorder to realize it's desired vision of becoming world class hub for aviation training.

On his side the NIT Resctor Eng.Dr.Prosper Mgaya thanked the Government of the United Republic of Tanzania under the leadership of the President Hon.Dr.Samia Suluhu Hassan for enabling NIT to reach the milestone.
"We are grateful to the Government for the tremendous support we have received, without their support we could not be able to attain this important achievement”.

National Institute of Transport - NIT

ππ€π“πˆπŽππ€π‹ πˆππ’π“πˆπ“π”π“π„ πŽπ… π“π‘π€ππ’ππŽπ‘π“ (ππˆπ“) ππ€π‘π“πˆπ‚πˆππ€π“π„π’ 𝐈𝐍 π€π…π‘πˆπ‚π€ π’πŠπˆπ‹π‹π’ π…πŽπ‘ π‰πŽππ’ ππŽπ‹πˆπ‚π˜ π€π‚π€πƒπ„πŒπ˜

Oct. 3, 2025, 9:47 a.m.

Nairobi, Kenya — 2nd October 2025.

The National Institute of Transport (NIT) is actively participating in the Africa Skills for Jobs Policy Academy, a four-day forum currently taking place in Nairobi, Kenya. The event, organized by the World Bank (WB) in partnership with the Inter-University Council for East Africa (IUCEA), began on 30th September 2025 and will conclude on 3rd October 2025.

Speaking during the forum, Eng. Dr. Prosper Mgaya, Rector of NIT, delivered an insightful presentation showcasing the transformative reforms and progress achieved under the East Africa Skills for Transformation and Regional Integration Project (EASTRIP). He highlighted key milestones, including the training and licensing of eight (8) Aircraft Maintenance Engineers, four (4) Cabin Crew, and eight (8) Pilots, alongside the acquisition of state-of-the-art training equipment and modern infrastructure to strengthen capacity in the aviation sector.

Dr. Mgaya also emphasized the Institute’s international recognition, notably from the International Air Transport Association (IATA) and the European Union Aviation Safety Agency (EASA). In addition, NIT has successfully secured four (4) Approved Training Organization (ATO) certifications, strengthening its position as a regional Centre of Excellence in Aviation and Transport Operations.

The Africa Skills for Jobs Policy Academy provides a critical platform for policy dialogue, knowledge exchange, and regional collaboration, with the goal of aligning Africa’s skills development agenda to the evolving needs of the labour market.

National Institute of Transport - NIT

πŒπŠπ”π” 𝐖𝐀 π‚π‡π”πŽ π€π™πˆππƒπ”π€ π‘π€π’πŒπˆ ππŽππ€ππ™π€ 𝐋𝐀 π–π€π…π€ππ˜π€πŠπ€π™πˆ ππˆπ“.

Oct. 3, 2025, 9:44 a.m.

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Mha.Dkt. Prosper Mgaya, amezindua rasmi Bonanza la Michezo la Wafanyakazi kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa NIT.

Bonanza hilo limefanyika Septemba 22, 2025, katika viwanja vya Chuo vilivyopo Mabibo jijini Dar es Salaam likihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa kikapu, kuvuta kamba, kufukuza kuku na mazoezi ya viungo vya mwili.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt. Mgaya alieleza kuwa lengo la bonanza hilo ni kuimarisha mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi, pamoja na kuchangia katika kuboresha afya na ustawi wa wanajumuiya wa NIT.

“Lengo letu ni kuongeza ari ya utendaji kazi kupitia michezo, afya njema na mshikamano baina ya watumishi na jamii ya Chuo kwa ujumla,” alisema Dkt. Mgaya.

Aidha, Dkt. Mgaya aliahidi kufanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa na Kamati ya Maandalizi ya bonanza hilo, hususa ni kuhusu ukarabati wa miundombinu ya michezo Chuoni .

Bonanza hili ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya mafanikio ya Chuo katika kutoa mafunzo mbalimbali katika sekta ya usafirishaji.

National Institute of Transport - NIT

ππˆπ“ π’πˆπ†ππ’ 𝐌O𝐔 π–πˆπ“π‡ π€π„π‘πŽπ“π„π‚π‡ππˆπ‚π’ 𝐋𝐓𝐃 π“πŽ 𝐄𝐍𝐇𝐀𝐍𝐂𝐄 π€π•πˆπ€π“πˆπŽπ π“π‘π€πˆππˆππ†

Oct. 3, 2025, 9:43 a.m.

Dar es Salaam, September 18, 2025 — The National Institute of Transport (NIT) has today signed a Memorandum of Understanding (MoU) with Aerotechnics Ltd, a leading company in the aviation industry, to enhance aviation training and expand global partnerships.

The agreement was signed at the Tibakweitira Council Chamber (NIT) in Dar es Salaam by NIT's Rector Eng. Dr. Prosper Mgaya, and the Board Chairperson of Aerotechnics Ltd, Eng.Jared Ajwang'a.

Speaking during the signing ceremony, Dr. Mgaya emphasized the significance of the partnership, stating:

“The agreement with Aerotechnics is aimed at enhancing aviation training at the institute to meet international standards in training delivery. This partnership will facilitate joint training programs that enable our students to obtain internationally recognized licenses, positioning NIT within the global aviation sphere and advancing aviation excellence at a global level. NIT is ready to establish programs that will enable our students to compete globally.”

On his part, the Board Chairperson of of Aerotechnics Ltd highlighted the importance of initiating strategic collaboration with NIT, noting:

“Through this partnership, we aim to advance aviation training at NIT to the global standard and the entire aviation industry. NIT has a strong foundation so we can help create globally certified and employable graduates. Our goal is to see NIT-trained professionals working across the world. This step marks the beginning of a strategic collaboration that will strengthen the aviation industry.”

The partnership is expected to lead to the establishment of joint training initiatives, exchange programs, and industry-standard certification courses, further cementing NIT’s role as a hub for aviation excellence in the region.