National Institute of Transport - NIT

LATEST NEWS

Fri, 30 Aug 2024 | 09:01 AM

NIT YATOA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA SHULE ZA MSINGI KUMI NA MOJA (11)

National Institute of Transport - NIT

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia kituo chake cha Umahiri cha Kikanda Katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kitengo cha Elimu ya Usalama Barabarani kimetoa Mafunzo ya Usalama Barabarani Mkoani Dodoma.

Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 28.8.2024 na 29.8.2024 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi kumi na moja(11) ikiwemo shule ya msingi Mazengo ,Kikuyu,Amani,Mlezi, Mlimani, Makole, Kizota, Chadulu, Mlimwa, na Kisasa.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wanafunzi hao uwelewa wa matumizi sahihi ya barabara.

Latest News

National Institute of Transport - NIT

๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—จ ๐— ๐—ž๐—จ๐—จ ๐—จ๐—–๐—›๐—จ๐—ž๐—จ๐—ญ๐—œ ๐—”๐—™๐—จ๐—ก๐—š๐—จ๐—” ๐—ž๐—œ๐—ž๐—”๐—ข ๐—–๐—›๐—” ๐—•๐—”๐—ฅ๐—”๐—ญ๐—” ๐—Ÿ๐—” ๐—ช๐—”๐—™๐—”๐—ก๐—ฌ๐—”๐—ž๐—”๐—ญ๐—œ ๐—ก๐—œ๐—ง ๐— ๐—ž๐—ข๐—”๐—ก๐—œ ๐——๐—ข๐——๐—ข๐— ๐—”

June 27, 2025, 5:41 p.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimefanya kikao cha kawaida cha Baraza la Wafanyakazi tarehe 27 Juni, 2025 katika Ukumbi wa Midland Inn View Hotel, Dodoma. Kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika Juni 26, 2025.

Kikao hicho kilifunguliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ambaye alikipongeza chuo kwa kuandaa vikao vinavyodumisha ushirikiano wa watumishi na uongozi. Alisisitiza kuwa NIT iendelee kuzalisha wataalamu kutokana na ukuaji wa sekta ya usafirishaji unaoletwa na miradi kama SGR na ongezeko la ndege za ATCL. Aidha, alihimiza ushirikiano na vyuo vya nje kwa ajili ya maendeleo ya kiteknolojia.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, Prof. Obadia Mbamba, alishukuru Wizara kwa ushirikiano wake unaosaidia ustawi wa chuo. Viongozi wa vyama vya wafanyakazi wa THTU na RAAWU Taifa waliupongeza uongozi wa NIT kwa maandalizi bora ya kikao na kutoa motisha kwa watumishi (incentive) inayoongeza morali ya kazi.

Mkuu wa Chuo, Dkt. Prosper Mgaya, alimshukuru Prof. Kahyarara kwa kuwa mgeni rasmi na kuahidi kuendeleza vikao hivyo kwa kuzingatia sheria na kanuni husika.

National Institute of Transport - NIT

๐๐ˆ๐“ ๐˜๐€๐“๐Ž๐€ ๐Œ๐€๐…๐”๐๐™๐Ž ๐˜๐€ ๐”๐’๐€๐‹๐€๐Œ๐€ ๐๐€๐‘๐€๐๐€๐‘๐€๐๐ˆ ๐Š๐–๐€ ๐Œ๐€๐ƒ๐„๐‘๐„๐•๐€ ๐–๐€ ๐•๐˜๐Ž๐Œ๐๐Ž ๐•๐˜๐€ ๐Œ๐Ž๐“๐Ž ๐Œ๐Š๐Ž๐€ ๐–๐€ ๐๐–๐€๐๐ˆ.

June 26, 2025, 11:29 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani (RCoERS), kimeanza kutoa mafunzo maalum ya usalama barabarani kwa madereva wa magari makubwa ya mizigo, daladala na bodaboda katika Mkoa wa Pwani.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 24 Juni, 2025 katika Stendi Kuu ya Mabasi ya Kibaha, Mkuu wa Kituo cha Umahiri cha Kikanda cha Usalama Barabarani – NIT, Ndg. Godlisten Msumanje, alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo madereva hao kutekeleza majukumu yao kwa weledi, huku wakizingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kulinda usalama wao pamoja na wa abiria wanaowahudumia.

“NIT imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji nchini kutoa elimu endelevu ya usalama barabarani kwa makundi mbalimbali katika jamii ili kuongeza uelewa wa usalama barabarani kwa watumiaji wote wa barabara,” alisisitiza Ndg. Msumanje.

Mafunzo haya yalianza rasmi tarehe 23 Juni, 2025 na yanatarajiwa kukamilika tarehe 27 Juni, 2025.

National Institute of Transport - NIT

๐Ÿฎ๐Ÿฌ ๐—ง๐—”๐—ก๐—ญ๐—”๐—ก๐—œ๐—”๐—ก ๐—ฆ๐—ง๐—จ๐——๐—˜๐—ก๐—ง๐—ฆ ๐—š๐—ฅ๐—”๐——๐—จ๐—”๐—ง๐—˜ ๐—™๐—ฅ๐—ข๐—  ๐—ก๐—œ๐—งโ€“๐—ž๐—œ๐—›๐—•๐—ง ๐—๐—ข๐—œ๐—ก๐—ง ๐—˜๐—ก๐—š๐—œ๐—ก๐—˜๐—˜๐—ฅ๐—œ๐—ก๐—š

June 26, 2025, 11:25 a.m.

oday, June 24, 2025, twenty (20) Tanzanian students graduated from a six-month joint engineering program between the National Institute of Transport (NIT) and the Kenya Institute of Highways and Building Technology (KIHBT) at the NIT Mabibo Campus.

Speaking during the graduation ceremony, Dr. Prosper Mgaya, Rector of NIT, announced that NIT and KIHBT formalized their partnership by signing a Memorandum of Understanding in October 2023 in Nairobi, Kenya. This collaboration operates under the umbrella of the World Bank's East Africa Skills for Transformation and Regional Integration Project (EASTRIP). Dr. Mgaya stated that following the signing, discussions focused on implementing a student exchange and mobility program to fulfill EASTRIP's requirement for regional enrollment in long-course programs.

On his side Dr. Chacha Ryoba, Center Leader of the NIT Center of Excellence in Transport Operations under EASTRIP, elaborated on the program structure. He stated that each institution enrolled twenty students in two distinct programs: Power Train and Suspension Systems and Construction Material and Testing.

NIT students completed a one-month in-person phase of the program in Kenya, followed by five months of online instruction delivered by KIHBT lecturers. Conversely, KIHBT students completed a one-month in-person phase in Tanzania, followed by five months of online instruction delivered by NIT lecturers. While the Kenyan students graduated on June 19, 2025, the Tanzanian students received their certifications today, June 24, 2025. The graduates expressed optimism and enthusiasm for their future endeavors in the engineering field.

50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025

Excellence in Transport for a Sustainable Economy.