National Institute of Transport - NIT
Bonyeza Kuthibitisha

ALL NEWS

All News

National Institute of Transport - NIT

ππˆπ“ π˜π€π“πŽπ€ πŒπ€π…π”ππ™πŽ π˜π€ π”π’π€π‹π€πŒπ€ ππ€π‘π€ππ€π‘π€ππˆ πŠπ–π€ πŒπ€πƒπ„π‘π„π•π€ 𝐍𝐀 πŒπ€πŠπŽππƒπ€πŠπ“π€ πŒπŠπŽπ€ 𝐖𝐀 πŠπ”π’πˆππˆ 𝐔𝐍𝐆𝐔𝐉𝐀

Aug. 30, 2024, 9:04 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani Zanzibar (ZARTSA) kimetoa mafunzo ya usalama barabarani kwa madereva na makondakta wa gari za abiria wa Mkoa wa Kusini Unguja.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku moja (1) yaliyofanyika tarehe 21.11.2024 Dunga Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia yale yote watakayojifunza ili kuondoa changamoto ya ajali za barabarani Zanzibar ambazo zimesababisha vifo na ulemavu kwa watu wengi.

Pia Mhe. Mahmoud ameushukuru Uongozi wa Chuo kwa kutoà mafunzo ya usalama barabarani kwa madereva na makondakta wa magari ya abiria katika Mkoa wa Kusini Unguja.

Naye Mkuu wa Kituo cha
Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani - NIT, Ndg. Godlisten Msumanje amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo madereva na makondakta juu ya matumizi sahihi ya barabara.

Kwa upande wa madereva na makonda waliyopatiwa mafunzo hayo wamekishukuru Chuo kwa kutoa mafunzo hayo na kuahidi kuzingatia yale yote waliojifunza ili kuboresha utendaji wa kazi zao.

National Institute of Transport - NIT

NIT YATOA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA SHULE ZA MSINGI KUMI NA MOJA (11)

Aug. 30, 2024, 9:01 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia kituo chake cha Umahiri cha Kikanda Katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kitengo cha Elimu ya Usalama Barabarani kimetoa Mafunzo ya Usalama Barabarani Mkoani Dodoma.

Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 28.8.2024 na 29.8.2024 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi kumi na moja(11) ikiwemo shule ya msingi Mazengo ,Kikuyu,Amani,Mlezi, Mlimani, Makole, Kizota, Chadulu, Mlimwa, na Kisasa.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wanafunzi hao uwelewa wa matumizi sahihi ya barabara.

National Institute of Transport - NIT

NIT YATOA MAFUNZO YA UDEREVA WA MAGARI YA MIZIGO (HGV)-DODOMA

Aug. 30, 2024, 8:59 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia kituo chake cha Umahiri cha Kikanda katika Usalama Barabarani (Regional Centre of Excellence for Road Safety) imetoa Mafunzo ya Udereva wa Magari ya Mizigo (HGV) kwa madereva kumi na nne (14).

Mafunzo hayo yameanza tarehe 19.08.2024 na yanatarajia kumalizika tarehe 31.08.2024 katika Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Mkoani Dodoma

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo na umahiri madereva hao katika kuendesha magari ya mizigo kwa kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani.

National Institute of Transport - NIT

π—‘π—œπ—§ π—¬π—”π—œπ—•π—¨π—žπ—” π— π—¦π—›π—œπ—‘π——π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—ͺ𝗔𝗑𝗭𝗔 π—žπ—ͺπ—˜π—‘π—¬π—˜ π— π—”π—’π—‘π—˜π—¦π—›π—’ 𝗬𝗔 π—žπ—’π—‘π—šπ—”π— π—”π—‘π—’ π—Ÿπ—” π—§π—œπ—¦π—” π—Ÿπ—” π—ͺπ—”π—›π—”π—‘π——π—œπ—¦π—œ π—ͺ𝗔𝗑𝗔π—ͺπ—”π—žπ—˜ π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—” (𝗧𝗔π—ͺπ—˜π—–π—˜)

Aug. 30, 2024, 8:57 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeibuka mshindi wa kwanza (1) kati ya Taasisi kumi na moja(11) za Elimu ya Juu ambazo zimeshiriki kwenye maonesho ya kongamano la tisa 9 la wahandisi wanawake Tanzania (Tawece) na kukabidhiwa tuzo ya mshindi wa kwanza.

Kongamano hilo limefanyika jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) kuanzia tarehe 21 hadi 22 Agosti,2024.

Mkuu wa Idara ya π™€π™‘π™šπ™˜π™©π™§π™€π™£π™žπ™˜π™¨ 𝙖𝙣𝙙 π™π™šπ™‘π™šπ™˜π™€π™’π™’π™ͺπ™£π™žπ™˜π™–π™©π™žπ™€π™£ π™€π™£π™œπ™žπ™£π™šπ™šπ™§π™žπ™£π™œ Bi. Grace Kibweja amepokea tuzo hiyo ya mshindi wa kwanza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo.

DIRISHA LA UDAHILI KWA NGAZI YA SHAHADA LIMEFUNGULIWA BONYEZA HAPA KUJISAJILI

July 17, 2024, 9:31 a.m.

National Institute of Transport - NIT

CPA AND CPSP REVIEW CLASSES REGISTRATION FORM

July 5, 2024, 2:03 p.m.

The National Institute of Transport (NIT) is offering intensive review classes to help you prepare for the Certified Public Accountant (CPA) and Certified Procurement and Supply Professional (CPSP) examinations in November 2024.

For registration, please click the link https://shorturl.at/sBYpq

 

For payment purposes contact the coordinators: 

Head CPD Mobile: +255713323370 or Assistant Head CPD Mobile +255719589955

Email: head.cpd@nit.ac.tz

 

 

National Institute of Transport - NIT

THE FIRST REGIONAL CENTRE OF EXCELLENCE FOR ROAD SAFETY IN EAST AFRICA KICKS OFF

June 22, 2024, 9:03 a.m.

National Institute of Transport - NIT

MAFUNZO YA WAHUDUMU WA MABASI YA MASAFA MAREFU NA MIJINI - DAR ES SALAAM

June 8, 2024, 10:41 p.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji chaendelea kutoa mafunzo kwa Wahudumu wa Mabasi ya Masafa Marefu na Mijini - Dar es salaam. Mafunzo hayo ya siku sita (6) yalianza siku ya Jumatatu tarehe 03.06.2024 na kuhitimishwa siku ya Jumamosi tarehe 08.06.2024 ambapo jumla ya washiriki 43 wemehudhuria mafunzo hayo na kutunukiwa vyeti.

Akizungumza na washiriki wakati wa Hafla ya Kufunga Mafunzo hayo iliyofanyika leo katika ukumbi wa Kituo cha Ukaguzi wa Magari uliyopo katika kampasi ya Chuo Mabibo jijini Dar es salaam, Kaimu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi, Dkt. John Mahona 
amewaasa washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia yale yote 
waliyojifunza ili kuleta tija na mabadiliko chanya katika vituo vyao vya kazi. Amesema

"Mkayazingatie yote mliyofundishwa ili kuleta tija katika vituo vyenu vya kazi"

National Institute of Transport - NIT

NIT students participated in a one day workshop organized by Carter Center in collaboration with China-Africa Vocational Education Cooperation Alliance (CAVECA)

June 8, 2024, 10:36 p.m.

NIT students participated in a one-day workshop organized by the Carter Center in collaboration with China-Africa Vocational Education Cooperation Alliance (CAVECA).

The workshop was held at NIT main campus Mabibo Dar es Salaam on Saturday 8th June 2024 focusing on empowering students with knowledge on the importance of climate - resilient infrastructure such as flood plains, embankments and other systems to reduce vulnerability to climate -related hazards such as floods and landslides.

KALENDA YA KOZI ZA MADEREVA JULY – DECEMBER 2024

June 7, 2024, 11:44 a.m.

STAND UP, SPEAK OUT, STOP CORRUPTION

Rushwa huzuia Maendeleo, Toa taarifa linda Haki.